WELCOME TO PROCUC SYSTEM

PROCUC SYSTEM | SWAHILI

Kichwa cha uvumbuzi: Procuc System                                                                                       
Jina la mvumbuzi: Marco Shigele

MAELEZO YANAYOHUSU UVUMBUZI
                                                                                                                               
Utangulizi
Mfumo wa Procuc ni mfumo mpya kabisa utakaokuwa msaada mkubwa sana katika biashara za ndani na nje. Mfumo huu utashawishi watu wengi sana kujiunga ili kuweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji.Wafanyabiashara wengi wataweza kupata fedha kwa ajili ya kukuza mitaji bila kukopa fedha kutoka taasisi yoyote ya fedha.Kwa hiyo watu watapata fursa ya kupata fedha kwa ajili ya kukuza mitaji yao bila dhamana ya kitu kisichohamishika.Mfumo wa Procuc ni tofauti kabisa na Upatu, kwa kuwa mfumo unamfanya mtu aweze kushiriki katika shughuli za uzalishaji badala ya kuchangiana pesa ambayo haitumiki moja kwa moja kwenye mzunguko wa kibiashara.Mfumo unalenga hasa kuwasaidia wafanyabiashara ambao hawana uwezo wa kukopa benki au taasisi yoyote ya fedha kwa kigezo cha dhamana ya kitu kisichohamishika. Pia mfumo huu unafaa hata kwa wafanyabiashara wenye uwezo wa kukopa benki au taasisi yoyote ya fedha.Vilevile, hata watu ambao si wafanyabiashara wataweza kupata mitaji kwa ajili ya kufanya biashara au kutekeleza malengo waliojiwekea kupitia mfumo huu.Mfumo wa Procuc unaweza kuwa hatua stahiki ya kuchukua kwa lengo la kupunguza umaskini kwa kuongeza uzalishaji,kuboresha huduma na kukuza ajira. Ikumbukwe kuwa mfumo huu hautaathiri kabisa shughuli za kibenki, badala yake utaiongezea benki wateja wenye sifa za kukopa kulingana na masharti ya kibenki na pia mfumo utaongeza uwezo na kasi ya kukuza uchumi wa Nchi.

Malengo ya mfumo wa Procuc
 Mfumo wa Procuc una malengo yafuatayo:
·         Kuongeza mtaji kwa biashara ambayo mtaji wake haukidhi haja ya wateja bila kukopa benki kwa kigezo cha dhamana ya kitu kisichohamishika.
·         Kuwawezesha watu wenye mtaji mdogo kuwa na uwezo wa kufanya biashara.
·         Kuwawezesha wafanyakazi ambao hawana muda wa kufanya biashara kwa sababu ya kubanwa na shughuli za kiofisi kuongeza kipato chao huku wakiendelea kufanya kazi.
·         Kuwanasua watu kutoka katika matumizi mabaya ya fedha.
·         Kuwashawishi watu wengi kushiriki katika shughuli za uzalishaji.



Matazamio ya Mfumo wa Prokak kwenye jamii
·         Mfumo unaweza kuzidisha umakini na uwajibikaji katika biashara.
·         Mfumo wa Procuc unaweza kuwa hatua stahiki ya kuchukua kwa lengo la kupunguza umaskini.

Dhana inayohusu mfumo wa Procuc
Mfumo wa Procuc ni njia inayotumika katika biashara ambayo inahusisha mwenye mali (Procuc Operator), mwenye hela (Customer) na mteja (Client). Jina Procuc limetokana na majina matatu yaliyotoholewa kutoka Lugha ya Kingereza ambayo ni Proprietor, Customer na Client. Herufi tatu za mwanzo (Pro) zinatokana na herufi tatu za mwanzo za jina Proprietor, cu inatokana na herufi mbili za mwanzo za jina Customer na c inatokana na herufi ya mwanzo ya jina Client.Kwa hiyo, Pro, cu and c kwa pamoja zinaunda jina Procuc. Mwenye mali, mwenye hela na mteja kwa pamoja wanajulikana kwa jina la wahusika wa mfumo wa Procuc. Elimu inayohusu mfumo wa Procuc inaitwa Procuciology. Mtu anayejifunza mambo yanayohusu Procuciology anaitwa Procuciologist.Mwanzilishi wa mfumo wa Procuc anaitwa Procusysiator.  

Wadau wa Mfumo wa Procuc
Kuna wadau watatu wa mfumo wa Procuc, ambao ni:-
·         Mwenye mali
·         Mwenye hela
·         Mteja

Mwenye mali
Katika mfumo wa Procuc, mwenye mali ni mtu anayeendesha biashara halali.Jina biashara katika mfumo huu linajulikana kwa jina la Procuc.Kwa hiyo, mwenye mali ni mtu ambaye anaendesha Procuc, pia ndiye mtu pekee anayetambuliwa rasmi katika uendeshaji wa Procuc.Procuc ni biashara inayofanyika kwenye mfumo wa Procuc au ni biashara yoyote au kitega uchumi chochote au mradi wowote ambao unaweza kuzalisha kiasi kikubwa cha faida kutokana na mtaji uliowekezwa. Mwenye mali ni mhusika wa kwanza wa mfumo wa Procuc.
           Mwenye hela
Mwenye hela ni mtu ambaye anaongeza hela (mtaji) kwenye mtaji wa mwenye mali ili kuweza kuendesha Procuc. Inawezekana kabisa kwa mwenye mali kuwa na watu  (wenye hela) wengi wa kumchangia mtaji.Mwenye hela ni mhusika wa pili wa mfumo wa Procuc.
          Mteja
Mteja ni mtu anayenunua bidhaa kwenye Procuc. Wateja wamegawanyika katika sehemu kuu mbili yaani wateja wa kwanza (umoja: mteja wa kwanza) na wateja wa pili (umoja: mteja wa pili).Mteja wa kwanza ni yule ambaye ananunua bidhaa kutoka kwa Pocu.Pocu ni jina la pamoja linalojumuisha , mwenye mali na mwenye hela.Kwa hiyo mtu akisema Pocu atakuwa ametaja majina mawili kwa pamoja, yaani mwenye mali na mwenye hela. Mteja wa kwanza kwa Pocu anaweza kuwa mwenye mali au baadaye akawa mwenye mali.Mteja wa pili ndiye mtumiaji wa mwisho wa bidhaa. Mteja ni mhusika wa tatu wa mfumo wa Procuc.
MWINGILIANO WA PROCUC
Mwingiliano wa Procuc (kwa kifupi mno, imeelezwa zaidi kwenye kitabu) unaonesha  jinsi mwenye mali na mwenye hela, mwenye mali na mteja wa kwanza, mwenye mali na mteja wa pili, Pocu na mteja wa kwanza, Pocu na mteja wa pili, mteja wa kwanza na mteja wa pili wanavyoweza kuhusiana katika kufanya biashara. Mwingiliano wao una faida kwa kila mmoja. Kuna aina sita za mwingiliano wa Procuc, aina hizo ni:-
·         Pocuism
·         Poconism
·         Poctism
·         Clieontism
·         Pocuclieonism
·         Pocuclientwism

 Pocuism
Pocuism ni mwingiliano kati ya mwenye mali na mwenye hela.Mwenye hela atapata fedha kutoka kwa mwenye mali. Fedha hiyo itatokana na kiasi cha hela ambacho yeye atakuwa amechangia kwenye Procuc. Mwenye mali atapata pesa kutokana na faida ya mtaji ambao Mwenye hela atakuwa amechangia kwenye Procuc.
       Poconism
Poconism ni mwingiliano kati ya mwenye mali na mteja wa kwanza. Mteja wa kwanza atapata manunuzi kutoka kwa mwenye mali.
              Poctism
Poctism ni mwingiliano kati ya mwenye mali na mteja wa pili. Mteja wa pili atapata manunuzi kutoka kwa mwenye mali.
             Clieontism
Clieontism ni mwingiliano kati ya mteja wa kwanza na mteja wa pili. Mteja wa pili atapata manunuzi kutoka kwa mteja wa kwanza.
             Pocuclieonism
Pocuclieonism ni mwingiliano kati ya Pocu na mteja wa kwanza. Mteja wa kwanza atapata manunuzi kutoka kwa Pocu.
          
Pocuclientwism
Pocuclientwism ni mwingiliano kati ya Pocu na mteja wa pili. Mteja wa pili atapata manunuzi kutoka kwa Pocu.

Masharti ya kuendesha Procuc
Ikumbukwe kuwa si kila biashara inafaa kuendeshwa kama Procuc wala si kila sehemu inafaa kwa Procuc. Vilevile si kila mtu anafaa kuwa mwenye mali.Kwa hiyo, Procuc inategemea mwenye mali, sehemu husika, mazingira ya kibiashara na aina ya biashara.Kwa sasa, katika kitabu cha Procuc System, kuna masharti kumi na saba yanayohusu uendeshaji wa Procuc.Masharti haya yana ainisha mambo manane ya msingi kama ifuatavyo:-
·         Sifa za mtu kuwa mwenye mali.
·         Sifa za mtu kuwa mwenye hela.
·         Mazingira ya kuendeshea Procuc.
·         Sifa ya Procuc.
·         Utaratibu wa malipo.
·         Muda wa kuendesha Procuc.
·         Utaratibu wa mtu kuwa mwenye hela.
·         Ukiukwaji wa mkataba baina ya mwenye mali na mwenye hela.

Kanuni za kihisabati
Kuna kanuni mpya za kihisabati ambazo zimevumbuliwa duniani kutokana na mfumo wa Procuc. Kanuni hizi zinaainisha jinsi malipo mbalimbali ya kifedha baina ya mweye mali na mwenye hela na kwa timu ya Procuc yatakavyofanyika katika mfumo huu.
Jinsi mfumo wa Procuc utakavyofanyika
Mfumo wa Procuc utafanyika kwa kuchangia Procuc kama ifuatavyo:-
Mwenye hela atapaswa kuchangia kiasi fulani cha hela kwenye Procuc kulingana na uwezo wake kwa malengo ya kujipatia faida kutokana na pesa aliyochanga. Mchango ambao mwenye mali anapaswa kuchangiwa na wenye hela ni asilimia themanini (80%) tu ya mtaji wake. Kwa mfano, kama mwenye mali ana mtaji wa Tshs. milioni tano (Tshs.5,000,000/=), anastahili kuchangiwa na wenye hela kiasi cha shilingi milioni nne (Tshs.4,000,000/=) tu.Kwa hiyo asilimia themanini ya mtaji wa mwenye mali inawezekana kabisa kurejeshwa kwa wenye hela. Faida ya mwenye hela inatokana na kisasi cha hela ambacho atakuwa amechangia kwenye Procuc. Kwa  mfano, endapo mwenye hela atachanga kiasi cha laki tano (Tshs.500,000/=), kama mtaji wake, kwa muda wa miezi tisa, faida yake itakuwa shilingi laki mbili thelathini na saba elfu na mia nne (Tshs.237,400/=).Faida hiyo inatokana na asilimia 0.52 (0.52%) kama kiwango ambacho kinatumika katika kukokotoa  kipato cha mwenye hela kwa siku na %CFP = 5%.Hata hivyo kiwango hicho cha asilimia kinaweza kubadilika kulingana na hali halisi ya gharama za maisha kwa kipindi hicho.Mabadiliko hayo hayatatokea kama tayari mkataba baina ya mwenye mali na mwenye hela umekwishatiwa saini kwa ajili ya kuendesha Procuc.Mkataba ukiisha, mwenye mali atarejesha mtaji pamoja na faida kwa mwenye hela.Baada ya marejesho, mwenye hela anaruhusiwa kutia saini mkataba mwingine kama yeye mwenyewe kwa hiari yake atahitaji kufanya hivyo.

USALAMA WA FEDHA YA MWENYE HELA (CUSTOMER’S FINANCIAL SECURITY)
Kabla ya kuainisha usalama wa fedha ya  mwenye hela, goja tuangalie mambo yafuatayo:-
·         Mchakato wa kumpata mwenye mali((kwa ufupi), -rejea maelezo zaidi kwenye kitabu).
·         Usimamizi wa Serikali, Benki na Timu ya mfumo wa Procuc katika mfumo wa Procuc.
·         Malipo ya mwenye hela

Mchakato wa kumpata mwenye mali (kwa ufupi)
Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa, Procuc inategemea mwenye mali, sehemu husika, mazingira ya kibiashara na aina ya biashara. Mwenye mali anapaswa kuwa na nyaraka  mbalimbali za biashara yake kama vile business license (for sole proprietors), certificate of incorporation (for companies), certificate of registration for Taxpayer Identification Number (TIN), Statement of Estimated Tax Payable for the Year of Income and inspection booklet.Vilevile anatakiwa kupata idhini kutoka serikalini ya kuendesha Procuc. Mchango ambao mwenye mali anapaswa kuchangiwa na wenye hela ni asilimia themanini (80%) tu ya mtaji wake. Ili mwenye mali aweze kuwalipa wenye hela malipo yao bila kusuasua, kila bidhaa anayoiuza lazima aiuze kwa faida ya asilimia thelathini (30%) mpaka asilimia arobaini (40%) ndani ya mwezi mmoja. Kwa mfano, kama bei ya kununulia bidhaa ni Tshs.1,000/=, bidhaa itauzwa kati ya Tshs.1,300/= mpaka Tshs.1,400/= au kama bei ya kununulia bidhaa ni Tshs.10,000/=, bidhaa itauzwa kati ya Tshs.13,000/= mpaka 14,000/= au katika kila milioni moja (Tshs.1,000,000/=), zinatakiwa Tshs.300,000/= mpaka Tshs.400,000/= kama faida ya mauzo ya bidhaa mbalimbali kwa mwezi. Kwa maana nyingine biashara inatakiwa kuwa na mzunguko mkubwa wa fedha kwa mwezi. Uzoefu wa mwenye mali katika biashara na historia ya madeni katika mfumo wa Procuc unahitajika kujulikana. Kwa nini yatupasa kufahamu uzoefu na historia ya madeni ya mwenye mali? Ili kuepuka kuanguka kwa biashara na kumnasua mwenye mali kuingia katika janga kubwa la kufilisika. Mtaji wa mwenye mali unapaswa kuwa mtaji ambao hautokani na madeni kutoka vyanzo vingine kama vile benki, taasisi za fedha au kwa watu binafsi. Endapo kama mwenye mali atakuwa na madeni kutoka vyanzo vingine vya fedha, hatapoteza sifa za kuwa mwenye mali, ingawa italazimika kukokotoa mtaji halisi ili aweze kupata mchango wa asilimia themanini (80%) tu ya mtaji wake kutoka kwa wenye hela.

Ikumbukwe kuwa, yapo baadhi ya mambo ambayo yanaweza kusababisha kuanguka kwa biashara kama vile matumizi mabaya ya fedha (yaani kutumia fedha zaidi kuliko uwezo wa mtu kiuchumi au kufurahia zaidi kabla ya muda husika), usimamizi mbovu katika biashara au ufuatiliaji hafifu katika kila kinachoendelea katika biashara, kushindwa kujipatia mtaji toshelevu, kuanzisha biashara kwa mkopo bila mtaji halisi, kumalizia kulipa deni la mkopo kwenye benki kwa kukopa pesa kutoka vyanzo vingine vya fedha na kutumia fedha ya mkopo katika mradi mwingine tofauti na maombi ya awali kuhusiana na mkopo. Katika mfumo wa Procuc, fedha kutoka kwa wenye hela, lazima itumiwe na mwenye mali katika mradi husika. Maana ikitumika vinginevyo, kuna uwezekano mkubwa kwa biashara kukwama au kuanguka kabisa. Kwa hiyo, uaminifu, umakini, uwajibikaji na elimu ya ujasiriamali ni baadhi ya mambo ya msingi katika ustawi biashara.    

 Usimamizi wa Serikali, Benki na Timu ya mfumo wa Procuc katika mfumo wa Procuc
Ili mfumo wa Procuc uweze kufanya kazi vizuri, ushirikiano mkubwa unapaswa ufanywe na Serikali, Benki na Timu ya mfumo wa Procuc.Ushirikiano wa vyombo hivi vitatu unaweza kuleta matunda kwenye mfumo. Vyombo hivi vina majukumu yafuatayo:
 Serikali
·         Kukusanya kodi ya mapato.
·         Kutoa ruzuku kwenye Procuc, hasa pale mwenye mali apatapo uwezo wa kujenga kiwanda.
·          Kutoa idhini kwa mwenye mali kuendesha Procuc.
Benki
·         Kurahisisha zoezi zima la kuendesha mfumo wa Procuc kwa kuwaunganisha mwenye mali na mwenye hela.Mwenye hela atakwenda Benki ili kumfahamu mwenye mali  ambaye anaendesha Procuc.Majina yote ya wenye mali  yatakuwa benki husika, kwa hiyo itakuwa rahisi kwa Benki kutoa huduma hiyo.
·         Kurahisisha zoezi la malipo kwenye akaunti ya mwenye mali na mwenye hela.
Timu ya mfumo wa Procuc
·         Kuelimisha jamii kuhusu mfumo wa Procuc.
·         Kufuatilia kwa ukaribu maendeleo ya Procuc zote.
Malipo ya mwenye hela (Customer’s financial payments)
Malipo ya mwenye hela yamegawanyika katika sehemu kuu mbili, ambazo ni:
·         Malipo ya kawaida ya mwenye hela (Customer’s normal financial payments)
·         Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina ya mwenye mali na mwenye hela (Customer’s financial payments due to tiocalization)
Malipo ya kawaida ya mwenye hela (Customer’s normal financial payments)
Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa, endapo mwenye hela atachanga kiasi cha laki tano (Tshs.500,000/=), kama mtaji wake, kwa muda wa miezi tisa, faida yake itakuwa shilingi laki mbili thelathini na saba elfu na mia nne (Tshs.237,400/=).Faida hiyo inatokana na asilimia 0.52 (0.52%) kama kiwango ambacho kinatumika katika kukokotoa  kipato cha mwenye hela kwa siku na %CFP = 5% . Kwa hiyo kipato chake kwa ujumla kitakuwa Tshs.737,400/=kwa kipindi cha miezi tisa. Hata hivyo si lazima mwenye hela kulipwa malipo yake kwa muda wa miezi tisa, kuna uwezekano wa kulipwa kwa muda tofauti kulingana na jinsi atakavyotia saini kwenye mkataba wakati wa mwanzo.
Jedwali lifuatalo, linaonesha jinsi ambavyo malipo ya kawaida ya mwenye hela yatakavyofanyika kwa nyakati tofautitofauti:
TND
y
ITND
CFT
CFP
in Tshs.
8.6
2
7
1Week
18,200
17.2
3
14
2weeks
36,400
34.25
4
30
1 Month
78,000
68.5
9
60
2 months
156,000
137
17
120
4 Months
312,000
274
4
270
9Months
702,000
Malipo kwa siku 270 ni Tshs. 702,000/= na kwa siku 274 ni Tshs.737,400/=
Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika kwa mkataba baina ya mwenye mali na mwenye hela (Customer’s financial payments due to tiocalization)
Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika kwa mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela (Customer’s financial payments due to tiocalization) yamegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni:
·         Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela-liosababishwa na mwenye mali (Customer’s financial payments due to tiocalization caused by a Procuc Operator)
·         Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela- liosababishwa na mwenye hela(Customer’s financial payments due to tiocalization caused by a Customer)
·         Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela - liosababishwa na Timu ya mfumo wa Procuc(Customer’s financial payments due to tiocalization caused by Procuc System Team)
Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika kwa  mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela-liosababishwa na mwenye mali (Customer’s financial payments due to tiocalization caused by a Procuc Operator)
Malipo ya mwenye hela kutokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina yake na mwenye mali -liosababishwa na mwenye mali yatategelemea kiwango cha asilimia (tiocalization percentage) alichojaza wakati wa kutia saini mkataba. Angalia jedwali lifuatalo:
The Procuc Operator Tiocalization Table for CGF drawn from CFC=Tshs. 500,000/=,  %CFPD = 0.52%, TND = 274 days and %CFP = 5%
Tiocalization Number (TN)
Tiocalization Percentage(TP)
in %
Incremental Percentage( )
in %
B
(i.e log10( ))
in %
P
in Tshs.
1
48
0.52
-0.283996656
740,000
2
49
1.52
0.181843587
745,000
3
50
2.52
0.40140054
750,000
4
51
3.52
0.546542663
755,000
5
52
4.52
0.655138434
760,000
6
53
5.52
0.741939077
765,000
7
54
6.52
0.814247595
770,000
8
55
7.52
0.87621784
7750,000
9
56
8.52
0.930439594
780,000
10
57
9.52
0.978636948
785,000
11
58
10.52
1.02201574
790,000
12
59
11.52
1.061452479
795,000
13
60
12.52
1.097604329
800,000
Where P stands for Customer’s payment due to tiocalization caused by a Procuc Operator and b stands for tiocalization exponent.
Malipo ya mwenye hela yanayotokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela- liosababishwa na mwenye hela(Customer’s payments due to tiocalization caused by a Customer)
Malipo ya mwenye hela kutokana na kuvunjika  kwa  mkataba baina yake na mwenye mali -liosababishwa na yeye mwenyewe yatafanyika kama ilivyoanishwa katika jedwali lifuatalo:
The table for CGF and I drawn from CFC=Tshs. 500,000/=, %CFPD = 0.52% and %CFP = 5% at various TNDs.
TND
NM
M
CGF in Tshs.
CFL in Tshs.
%CFL
CI in Tshs.
I=CGF+CI
in Tshs.
30
1
November-30
103,000
397,000
79.4
9819.33
112819.33
61
2
December-31
183,600
316,400
63.28
18384.48
201984.48
92
3
January-31
264,200
235,800
47.16
19480.35
283680.35
121
4
February-29
339,600
160,400
32.08
16481.92
356081.92
152
5
March-31
420,200
79,800
15.96
35016.67
455216.67

182
6
April-30
498,200
1800
0.36
     -
     -
213
7
May-31
578,800
     -
     -
     -
     -
243
8
June-30
656,800
     -
     -
     -
     -
274
9
July-31
737,400
     -
     -
     -
     -


Usalama wa fedha ya mwenye hela (Customer’s Financial Security)
Kwa kuwa kiwango anachotakiwa kuchangiwa mwenye mali kutoka kwa wenye hela ni asilimia themanini (80%) tu ya mtaji wake, kiwango hicho kinawezekana kabisa kurejeshwa kwa wenye hela pamoja na riba yake. Kwa mfano, kama mwenye mali anamtaji wa shilingi milioni mia tano (Tshs.500,000,000/=), mchango kutoka kwa wenye hela utakuwa shilingi milioni mia nne (Tshs.400,000,000/=) na kuufanya mtaji wa mwenye mali kuwa mlioni mia tisa (Tshs.900,000,000/=). Endapo asilimia 0.52 kama kiwango ambacho kitatumika katika kukokotoa kipato cha wenye hela kwa siku na %CFP=5%, faida itakayotokana na milioni mia nne kama mtaji wa wenye hela kwa kipindi cha miezi tisa itakuwa shilingi milioni mia moja themanini na tisa, laki tisa na elfu ishirini (Tshs.189,920,000/=). Kiwango hiki cha pesa ni sawa na ongezeko la asilimia 47.48 ya mtaji wa wenye hela. Pia ongezeko hilo ni sawa na asilimia 37.984 ya mtaji wa mwenye mali. Chukulia kwamba mwenye mali anafanya biashara bila ya yeye kupata faida, ila fedha zinazopatikana ni kwa ajili ya kuwalipa wenye hela tu, ukweli ni kwamba mtu huyu ataweza kurejesha fedha hizo. Kwa mfano, katika milioni mia nne (Tshs.400,000,000/=), kila mioni moja (Tshs. 1,000,000/=) inatakiwa kuwa na faida ya shilingi laki nne, sabini na nne elfu na mia nane (Tshs.474,800/=) kwa kipindi cha miezi tisa. Kiwango hicho cha faida kinakadiriwa sawa na shilingi hamsini na tatu elfu (Tshs.53,000/=) katika kila milioni moja kwa mwezi. Hebu tujiulize, hivi, inawezekana kweli  katika kila milioni moja kukosekana laki nne sabini na nne elfu na mia nane(Tshs.474,800/=)  kwa miezi tisa au  shilingi hamsini na tatu elfu (Tshs.53,000/=) kwa mwezi kwa ajili ya kuwarejeshea fedha zao wenye hela? Jibu, la hasha!
Kwa kuwa timu ya mfumo wa Procuc itakuwa na mamlaka ya kufuatilia kwa ukaribu maendeleo ya Procuc zote, ikionekana kuwa kuna kila dalili kwa mwenye mali kuanza kupata hasara katika biashara yake, itavunja mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela ili kuweza kuokoa upotevu wa fedha katika pande zote mbili, na itafanya hivyo kwa kushauriana na Serikali pamoja na Benki husika. Hata kama timu ya mfumo wa Procuc itaingilia kati mkataba baina ya mwenye mali na mweye hela, sharti, mwenye mali lazima atalazimika kumlipa mwenye hela kiasi fulani cha riba na mwenye hela atalazimika kulipa mutable amount.Kwa hiyo, katika mazingira hayo fedha ya mwenye hela itakuwa salama kabisa.
Customer’s entry fee (kiingilio cha mwenye hela) and Mutable amount
Mwenye hela atapaswa kutoa kiingilio kabla ya kuanza mkataba au siku ya kuanza mkataba, kiingilio hicho kitawezesha shughuli zote za kibenki kutekelezwa.Vilevile atapaswa kutoa kiasi kidogo kiitwacho “mutable amount” siku ya kumaliza mkataba.Mutable amount itaiwezesha timu ya mfumo wa Procuc kujiendesha au kutimiza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.


 FAIDA YA MFUMO WA PROCUC KWA SERIKALI NA BENKI
Serikari itakusanya kodi kubwa kutoka kwa wenye mali kwa kuwa kipato cha wenye mali kitazidi kuongezeka. Vilevile Serikali itakusanya kodi kwa wenye hela pale watakapopata uwezo wa kuanzisha biashara zao wenyewe baada ya kupata mtaji kutokana na mfumo wa Procuc. Benki zitaweza kupata wateja wenye sifa ya kukopa kwa dhamana (collateral).

ISTILAHI
Kuna Istilahi mpya ambazo zimepatikana kutokana na mfumo wa Procuc. Istilahi hizi zimetokana na Lugha ya Kiingereza na pia matamshi yake yanapatikana kwenye kitabu.

KITABU 
Mfumo wa Procuc umepelekea kuandika kitabu kiitwacho “PROCUC SYSTEM”. Kitabu hiki kina sura nne ambazo ni:
·         Introduction to Procuc System
·         Procuc Operation and Business units
·         Poculization and Procuclization
·         Let us invest in Tanzania. 
Utendaji kazi wa Procuc unategemea sana matumizi ya mashine ziitwazo “Electronic Fiscal Devices (EFDs)”, kwa hiyo, maelezo kuhusu matumizi ya mashine hizo yameelezwa kwa kina kwenye kitabu hicho.Fursa mbalimbali za uwekezaji kama vile kilimo, viwanda, madini, utalii, biashara, nishati, uchukuzi, teknohama n.k.vimeelezewa ndani ya kitabu.Nunua kitabu uone jinsi mfumo ulivyo naTanzania ilivyotajiri.Pia Monetary units za nchi mbalimbali duniani zimeandikwa kwenye kitabu.Hii itawapa fursa watu wanaosafiri kwenda nchi mbalimbali duniani kufahamu pesa inayotumika katika nchi husika kabla ya kuanza safari.             
Kwa ufupi, nunua kitabu cha Procuc System, ujifunze mambo yafuatayo:
·         Dhana inayohusu mfumo wa Procuc
·         Wadau wa Procuc
·         Mwingiliano wa Procuc
·         Triple Mechanism Model (TMM)
·         The fundamental raison d’être of Procuc System
·         Masharti ya jumla kwa ajili ya kupata mkopo kutoka kwenye benki
·         Jinsi mfumo wa Procuc utakavyofanyika
·         Masharti ya kuendesha Procuc
·         Umuhimu wa mfumo wa Procuc
·         Makundi ya watu au watu wenye sifa za kuendesha Procuc
·         Makundi ya watu au watu ambao hawastahili kuendesha Procuc
·         Matumizi ya mashine ziitwazo “Electronic Fiscal Devices (EFDs)” katika mfumo wa Procuc
·         Financial transaction
·         Commercial transaction
·         Business units (Sole proprietorship, Partnership, Joint stock companies (Public limited company and Private limited company), Cooperatives, Public corporation, Local authorities and Parastatal bodies)
·         Mlandano na tofauti kati ya mfumo wa Procuc na Business units zingine
·         Dhana inayohusu poculization na procuclization
·         Dhana inayohusu proeperio, prosperio na tiocalization
·         Exponential Principle of Poculization
·         Kanuni mpya za kihisabati
·         Monetary units
·         Uwekezaji, mazingira ya uwekezaji, sababu za kuwekeza na fursa za uwekezaji Tanzania.

ONYO: NI MARUFUKU KUANZA KUTEKELEZA MFUMO WA PROCUC BILA YA
              TAMKO LA SERIKALI.

No comments:

Post a Comment